Mkuu wa Trafiki Mkoa wa Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi wa Polisi Awadhi Haji ameendelea kutembeklea vituo mbalimbali vya Bajaji na Bodaboda jijijni katika juhudi za Jeshi la Polisi kupunguza kama si kuondoa kabisa ajali za barabarani. ACP Awadhi leo ametembelea kituo cha Africa sana eneo la Sinza na kutoa elimu ya usalama barabarani kwa madereva wa vyombo hivyo vy abiria, akiwataka kuzingatia na kufuata sheria za usalama barabarani pamoja kuhakikisha wanatengeneza pikipiki zao ili ziwe katika ubora wa kubeba abiria. Madereva hao wamefurahia hatua ya kamanda huyo kupita kila pembe ya jiji kutoa elimu, wakisema hatua hiyo ni ya kutia moyo kwani inaimarisha uhusiano mwema kati yao na wana usalama barabarani.
 Mkuu wa Trafiki Mkoa wa Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi wa Polisi Awadhi Haji akielezea umuhimu wa kuwa na Bajaji na Bodaboda zisizo na hitilafu ili kuhakikisha usalama wa abiria
 Mkuu wa Trafiki Mkoa wa Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi wa Polisi Awadhi Haji akisisitiza umuhimu wa kuvaa helmet kwa dereva pamoja na abiria
Mkuu wa Trafiki Mkoa wa Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi wa Polisi Awadhi Haji akikagua uimara wa Bodaboda

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...