Kocha Mkuu wa timu ya Tanzania, Salum Mayanga (pichani) leo Ijumaa  Machi 19, 2017 ametangaza majina ya wachezaji 24 watakaounda kikosi hicho cha Timu ya Taifa Stars ambacho sasa kinachodhaminiwa na Kampuni ya Bia ya Serengeti.

Katika mkutano na wanahabari uliofanyika Makao Makuu ya TFF, yaliyoko Uwanja wa Karume, Ilala jijini Dar es Salaam, Mayanga alisema kikosi hicho kinaundwa na makipa Aishi Manula  (Azam FC), Benno Kakolanya  (Yanga SC) na Said Mohammed (Mtibwa Sugar). 

Walinzi wa pembeni upande wa kulia aliwataja Shomari Kapombe    (Azam FC) na Hassan Kessy (Yanga SC) wakati upande wa kushoto wapo Mohammed Hussein (Simba) na Haji Mwinyi  (Yanga SC). 
Mayanga aliwataja walinzi wa kati Erasto Nyoni  (Azam FC), Salim Mbonde (Mtibwa Sugar), Abdi Banda (Simba SC) na Aggrey Morris  (Azam FC) ilihali aliwataja viungo wa kuzuia kuwa ni Himid Mao (Azam FC) na Jonas Mkude (Simba SC). 
Kadhalika wako viungo wa kushambulia Salum Abubakar (Azam FC), Said Ndemla  (Simba SC) na Muzamiru Yassin (Simba) wakati viungo wa kulia waliotajwa ni Simon Msuva (Yanga SC) na Shizza Kichuya (Simba SC). 
Viungo wa kushoto ni Farid Mussa (Teneriffe, Hispania)  wakati washambuliaji ni Mbwana Samatta (KRC Genk- Ubelgiji), Thomas Ulimwengu (AFC Eskilstuna – Sweden), Ibrahim Ajib (Simba SC), Mbaraka Yusufu (Kagera Sugar) na Abdurahman Mussa (Ruvu Shooting).
Pia Mayanga aliwataja wasaidizi wake kuwa ni Kocha Msaidizi kuwa ni Novatus Fulgence  wakati Kocha wa Makipa, Patrick Mwangata wakati Meneja wa atakuwa Danny Msangi; Mtunza Vifaa, Ally Ruvu wakati Daktari wa timu atakuwa Richard Yomba huku Daktari wa viungo   akiwa ni Gilbert Kigadya. 

Timu hiyo itaingia kambini Machi 23, 2017 kwenye Hoteli ya Urban Rose, Dar es Salaam mpaka tarehe 29 baada ya hapo itasafiri kwenda Misri kwa kambi ya wiki moja kabla ya kurejea kuja kucheza mchezo wa kufuzu Mataifa huru ya Afrika mchezo  na Lesotho, mchezo utachezwa Tarehe 10  mwezi wa 6 mwaka huu jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...