Kamati ya Uchaguzi inachukua fursa hii  kuwataarifu Watanzania wote waishio Reading na maeneo ya jirani ya kuwa  tutakuwa na *mkutano mkuu wa kuwachagua viongozi wa jumuiya yetu hapa Reading ni siku ya JUMAMOSI TAREHE 29/07/2017 kwa yoyote yule atakayependa kuwania nafasi   basi unatakiwa kujaza fomu na kuirejesha mapema iwezekanavyo.
Pia kwa wale ambao hawatakuwa na uwezo wa ku download fomu ya kugombea Uongozi, basi mnaomba mwasiliane na sisi ili tuweze kuwatumia hard copy.
Upatapo ujumbe huu basi mjulishe na mwenzako, Fomu zirudishe kwenye email ya Kamati ya uchaguzi kama ilivoahinishwa hapo chini.
Pia kwa ufafanuzi au maswali yoyote yale basi usisite kuwasilaina na kamati ya uchaguzi kwa njia ya barua Pepe tajwa hapa chini.Watanzania wote wanaoishi Reading na maeneo ya jirani mnakaribishwa kuja kuchagua Viongozi wenu.
Tuma maombi yako ya kugombea Uongozi au ufafanuzi kwa barua pepe kwenda
NAFASI ZA KUGOMBEA 
NGAZI YA JUU YA UONGOZI
1:Mwenyekiti
2:Makamu Mwenyekiti
3:Katibu
4:Katibu Msaidizi
5:Mtunza Hazina/Mtunza Hazina Msaidizi
WAJUMBE
Kuna nafasi nne za wajumbe  ambazo zinatakiwa kujazwa siku hiyo.
     UCHAGUZI : 29/07/2017
MUDA: Kuanzia saa Kumi kamili jioni (4.00pm)
UKUMBI
Bridge  Hall
Oxford Road
 Reading
 Berkshire
 RG1 7PL
MUDA : 10.00 jioni - 3.30usiku (4.00pm - 9.30pm). Mara baada ya Uchaguzi kutakuwa na Chakula, Vinywaji na Burudani Kidogo. Wasiliana na sisi kwa njia ya email tajwa hapo juu au simu nambari 07402 344004
Umoja ni Nguvu, Pamoja Tunaweza!
Tangazo hili limeletwa kwenu na Kamati ya Uchaguzi TA  Reading 2017.
Tanzania Association Reading
WOTE MNAKARIBISHWA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...