Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii

Baada ya Matokeo ya Kidato cha Sita , Global Education Link (GEL) ambao ni mawakala wa Vyuo Vikuu vya Nje imesema kuwa wanafunzi wanaotaka kujiunga na vyuo vikuu vya nje udahili ni papo kwa papo na vyuo hivyo viko wazi.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Global Education Link (GEL), Abdulmalik Mollel amesema katika azma ya serikali ya awamu ya tano ya viwanda, inahitaji rasilimali watu ya kutosha ambao ndio watasukuma gurudumu hilo la viwanda na ujuzi upo katika vyuo vya nje ambapo nchi zenye vyuo vina uatajiri wa viwanda.

Mollel amesema kuwa vyuo ambavyo anashirikiana na vina uwezo wa kutosha katika uzalishaji wa rasilimali watu katika sekta ya viwanda.Amesema kuwa wazazi wanaotaka kupeleka wanafunzi katika vyuo vikuu vya nje hawatajutia kutokana na mazingira wanayokwenda kusoma huko.

Mollel amesema kuwa wazazi na wanafunzi wafike katika ofisi zao ziko katika mikoa ya Dar es Salaam viwanja vya Saba saba , Dodoma , Mbeya, Mwanza, Zanzibar, Arusha pamoja na nchi ya Zambia.

Amesema kuwa mwanafunzi atayekuwa anapitia katika wakala hiyo atapata uangalizi kwa muda wote masomo yake katika kuhakikisha mzazi kile anachokifanya kwa kijana wake hawezi kujutia.

Mollel amesema kuwa wazazi na wanafunzi wanaweza kufika katika ofisi zao kwa maelezo na jinsi kuwafanyia udahili wa papo kwa papo.
Mkurugenzi wa Global Education Link (GEL), Abdulmalik Mollel akizungumza na wateja waliofika kupata huduma katika ofisi za Global Education Link zilizopo katika viwanja vya sabasaba jijini Dar es Salaam.
Afisa Masoko wa Global Education Link (GEL) Damaricy Peter akiwapa maelekezo wateja waliofika kupata huduma katika ofisi za Global Education Link zilizopo katika viwanja vya sabasaba jijini Dar es Salaam.
Afisa wa Hati ya Kusafiria Passport , Abdul Milanzi akimsainisha fomu ya hati ya kusafiria mteja wa Global Education Link GEL leo katika ofisi za Global Education Link zilizopo katika viwanja vya sabasaba jijini Dar es Salaam.
Meneja Masoko wa Chuo Kikuu cha Lovely Professional, Love Kumas akizungumza na mteja katika ofisi za Global Education Link (GEL) leo jijini Dar es Salaam.picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...