Walimu wa masomo ya Sayansi mkoani Lindi wameiomba Serikali kuchukua hatua za haraka za kuandaa na kuimarisha miundombinu bora kwa shule za Sekondari zinazofundisha masomo hayo ili kuendeleza na kufufua vipaji vya wanafunzi.

Akizungumza kwa niaba ya walimu hao wakati wa ziara iliyofanywa na wahandisi wa kike kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), kupitia Kitengo maalum cha ushirikishwaji wa wanawake katika masuala ya barabara katika shule za mkoa huo,   Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Mchinga iliyopo  mkoani humo, Bw. Makopa Selemani , amesisitiza kwa Serikali kuona namna ya kujenga maabara  nyingi za sayansi ambazo zitakuwa na vifaa na kuongeza walimu wa Sayansi ambao wameonekana kuwa ni wachache katika mkoa huo.

"Tunaiomba Serikali kutazama kwa jicho la pekee shule za mkoa huu hususan zenye michepuo ya sayansi kwani si kwamba wanafunzi hawapendi masomo haya bali miundombinu hairidhishi", amesema Mwalimu Mkuu.
Aidha, Mwalimu Mkuu ameongeza kuwa ili kuwasaidia wanafunzi wa kike katika mkoa huo serikali iwajengee mabweni wanafunzi hao ili kuepusha kupata vishawishi kwani wengi wao wanaishi mbali na shule.

Mwalimu Mkuu Selemani, ameelezea baadhi ya mikakati ya shule yake katika kuhamasisha wanafunzi wa kike kusoma masomo ya sayansi ikiwemo kufanya vikao vya mara kwa mara na wanafunzi hao ili kujadili changamoto zao na kuzitatua.
 Mhandisi kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Kitengo maalum cha ushirikishwaji wa wanawake katika masuala ya barabara, Bi. Liberatha Alphonce, akionesha mfano wa picha iliyochorwa kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Mchinga mkoani Lindi (hawapo pichani), ili kuhamasisha wanafunzi kupenda masomo ya sayansi.
 Wahandisi kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Kitengo maalum cha ushirikishwaji wa wanawake katika masuala ya barabara, wakisikiliza maoni kutoka kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Mchinga mkoani Lindi walipotembelea shule hiyo kuhamasisha usomaji wa masomo ya Sayansi kwa wasichana.
 Baadhi ya Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Mchinga mkoani Lindi, wakionesha ndoto zao kwa Wahandisi wa kike kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Kitengo maalum cha ushirikishwaji wa wanawake katika masuala ya barabara, walipotembelea shule hiyo kuhamasisha usomaji wa masomo ya Sayansi kwa wasichana.
Mhandisi kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Kitengo maalum cha ushirikishwaji wa wanawake katika masuala ya barabara, Bi. Rahma Mwinyi, akigawa zawadi ya madaftri kwa wanafunzi wa shule ya Mkonge mkoani Lindi ili  kuhamasisha wanafunzi  hao kupenda masomo ya sayansi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...