Waziri
wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt.Harrison Mwakyembe akizungumza
na wajumbe wa Kamati ya Maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Kimataifa wa
Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA) (hawapo pichani) unaotarajia
kufanyika nchini mwezi Februari 2018 kuhakikisha maandalizi yanakuwa
mazuri ili ujio huo uwezekuletea manufaa kwa taifa katika kikao
kilichofanyika jana jijini Dar es Salaam
Wajumbe
wa Kamati ya Maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Kimataifa wa Shirikisho la
Mpira wa Miguu Duniani (FIFA) wakisililiza maagizo ya Waziri wa Habari
Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt.Harrison Mwakyembe aliyokuwa akitoa
katika kikao hicho kwa lengo la kufanikisha ujio huo wa Kimataifa kuwa
unaleta manufaa kwa taifa jana jijini Dar es Salaam.
Baadhi
ya Wajumbe wa Kamati ya Maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Kimataifa wa
Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA) wakifuatilia maelekezo
yaliyokuwa yanatolewa na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo
Dkt.Harrison Mwakyembe katika kikao cha maandalizi ya ujio huo
kilichofanyika jana jijini Dar es Salaam,wapili kulia ni Mkurugenzi wa
Idara ya Maendeleo ya Michezo kutoka Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na
Michezo Bw. Yusuph Singo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...