*Aishukuru Serikali,SIDO kwa kutambua mchango wa kiwanda
chake cha virutubisho tiba

Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

MKURUGENZI wa Kampuni ya Fadhaget inayomiliki kiwanda cha Virutubisho Tiba Fadhaget Nutrition Science, Dkt Fadhili Emily ameishukuru Shirika la Kuhudumia Viwanda vidogo vidogo(SIDO) pamoja na Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dk.John Magufuli kwa kuwaona vijana wa Tanzania kuwa wanao uwezo wa kumiliki viwanda.

Amesema kuwa kauli ya Rais Magufuli imewafanya vijana wajikwamue na umasikini uliokithiri na sasa wigo wa ajira unaendelea kuongezeka kutikana na viwanda vinavyoanzishwa kutokana na dhamira njema ya Serikali inavyohimiza ujenzi wa viwanda.

Amesema hayo wakati anazungumzia na Michuz Blog baada ya SIDO kumtunuku cheti cha kutambua kiwanda chake na mchango ambao anautoa katika kuelekea nchi ya viwanda ambapo cheti hicho amekabidhiwa jana."Sisi kama kiwanda cha kwanza Tanzania cha kuandaa virutubisho tiba vyenye uwezo wa kupambana na magonjwa mbalimbali ya mfumo wa mwanadamu tunaahidi kuzalisha mara dufu ili kuhakikisha watu wanapatapa kilicho bora zaidi kutoka Fadhaget Nutrition Science,"amefafanua.

Akifafanua zaidi kuhusu Fadhaget Nutrion Science,Fadhili  amesema wamekuwa wakiandaa virutubisho tiba kwa njia za kisasa kabisa kwa kuzingatia kanuni za usalama wa vyakula na virutubisho duniani yaani HACCP(Hazard Analysis and Critical Control Point).Amesema furaha yao ni kuhakikisha watu wanatapa tiba salama isiyo na madhara ya baadae na wamefanikiwa baada ya kuandaa virutubisho kwa magonjwa karibia yote hasa yale ya virusi vya magonjwa ya muda mrefu.

Ametaja baadhi ya magonjwa hayo ni Ukimwi, vidonda vya tumbo, U.T.I sugu, malaria sugu ,upungufu wa nguvu za kiume, figo , ini, kifua kikuu , pumu (arthima), kisukari, matatizo ya uzazi pande zote yaani kutopatikana mtoto katika ndoa , uvimbe wa kizazi na kuziba kwa mirija ya kizazi ."Pia magonjwa ya zinaa na dalili nyngine nyingi za hatali kiafya kama vile miguu kufa ganzi , miguu kuwaka moto, miguu kuvimba na unapoibonyeza lina baki shimo kama unavyobonyeza ndizi mbivu.

"Kuwashwa ukeni kwa akina mama na kutokwa na uchafu mzito mweupe katika via vya uzazi au wa kahawia wenye harufu na unapopata mkojo unakuwa wa njano sana ikiwa ni pamoja na matatizo ya kukosekana kwa hamu ya tendo la ndoa,"amesema.Kuhusu cheti ambacho amepewa na SIDO cha kutambua kiwanda chake amesema kama kijana wa Kitanzania atahakikisha cheti hichi kinakumbusha kuwa analo jukumu la kuunga mkono juhudi za Rais Dk.Magufuli ya kuwa na Tanzania ya viwanda na kwake na kuongeza itakuwa chache kwake kuzalisha bidhaa zenye ubora wa hali ya juu kwa maslahi ya Watanzania wote.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Fadhaget inayomiliki Kiwanda cha
Virutubisho Tiba Fadhaget Nutrition Science (kushoto),Fadhili Emily  akipokea cheti kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Kuhudumia Viwanda vidogo vidogo(SIDO).Cheti hicho ni kwa ajili ya kutambuliwa kwa kiwanda chake ambacho amekabidhiwa leo jijini Dar es Salaam.
 



Cheti ambacho amekabidhiwa Mkurugenzi wa Kampuni ya Fadhaget inayomiliki Kiwanda cha Virutubisho Tiba Fadhaget Nutrition Science kutoka Shirika la kuhudumia Viwanda vidogo vidogo(SIDO).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...