Na Ripota Wetu, China
BALOZI wa Tanzania nchini China Mbelwa Kairuki amesema zaidi
watu 1,000 wamepata fursa ya kutembelea banda la
Tanzania ambalo lilikuwepo kwenye maonesho ya utalii nchini
humo.
Idadi hiyo ya watu ambao wametembelea banda la Tanzania
imesaidia kuwapatia taarifa sahihi na za kutosha kuhusu utalii
wetu na ni moja ya eneo ambalo limetumika vema kutangaza
vivuto vilivyopo.
Balozi Kairuki ametoa kauli hiyo wakati akizungumza kwenye
maoesho ya utalii yaliyofanyika nchini China ambayo yamemalizika
hivi karibuni.
Akifafanua zaidi kuhusu Maonyesho ya biashara ya Utalii (China
Outboard Travel & Tourism Market COTTM) yaliyomalizika hivi
karibuni jijini Beijing China Balozi Kairuki amesema maonesho
hayo yamekuwa na mwitikio mkubwa.
"Zaidi ya watu 1,000 wameweza kutembelea banda la Tanzania
hatua ambayo imesadia watu wengi kupata taarifa za kutosha
kuhusu fursa za Tanzania.Naipongeza bodi ya utalii na mamlaka
zote za utalii Tanzania pamoja na mawakala wa utalii ambao
walishiriki kwa lengo la kuchangamkia fursa hiyo,"amesema.
Ameogeza soko la China ni jipya na linalokua kwa kasi,hivyo
matarajio yao hizo taasisi za bodi ya utalii, Hifadhi ya Ngorongoro
,TANAPA watapewa nguvu zaidi, watawezeshwa kibajeti ili
wakushiriki maonyesho mengi zaidi hapa China.
Balozi wa Tanzania nchini China, Mbelwa Kairuki (Kushoto) akishiriki mahojiano maalumu yaliyolenga kutangaza Vivutio vya Utalii na Utamaduni wa Tanzania kupitia kituo cha runinga cha "Chinese Satelite Travel" chenye watazamaji zaidi ya Milioni 100 ndani na nje ya China. Mahojiano hayo yaliongozwa na Bi. Mei Qing mtangazaji maarufu wa Television hiyo.
Afisa Utalii kutoka Hifadhi ya Ngorongoro, Piter Makutian (Kushoto) akizungumza jambo katika mahojiano maalumu yaliyolenga kutangaza Vivutio vya Utalii na Utamaduni wa Tanzania kupitia kituo cha runinga cha "Chinese Satelite Travel" chenye watazamaji zaidi ya Milioni 100 ndani na nje ya China. Mahojiano hayo yalifanyika wakati wa Maonyesho ya Utalii yaliyofanyika Beijing China mapema wiki hii. Kulia ni Balozi wa Tanzania nchini China, Mbelwa Kairuki.
Mahojiano yakiendelea yaliyolenga kutangaza Vivutio vya Utalii na Utamaduni wa Tanzania kupitia kituo cha runinga cha "Chinese Satelite Travel"
Balozi wa Tanzania nchini China, Mbelwa Kairuki(katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kumalizika kwa mahojiano kwenye kituo cha runinga cha "Chinese Satelite Travel"
Balozi wa Tanzania nchini China, Mbelwa Kairuki(kushoto) akipata maelezo kuhusu Maonyesho ya Utalii kutoka kwa Afisa Utalii Mwandamizi - Hifadhi ya Taifa Tarangire Theodora Aloyce (katikati), Wa pili kushoto ni Afisa Utalii habari - Bodi ya Utalii Tanzania, Irene Mville, Afisa Utalii- Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro, Piter Makutian (wa pili kulia) na Afisa Kutoka Ubalozi wa Tanzania nchini China, Lusekelo Gwassa
Katibu
Mkuu wa Shirikisho la Wanafunzi Watanzania nchini China, Remidius
Emmanuel(Kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji
wa Kampuni ya Compass Safari, Peter Larocque inayofanya kazi zake nchini
Tanzania.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...