Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba akifungua kongamano la vijana kutoka Vyuo vya Elimu ya Juu vilivyopo mkoani Dodoma. Jumla ya Vyuo sita vimeshiriki katika Kongamano hilo lililofanyika katika Chuo cha Mipango, Dodoma na mada kuu ikiwa ni fursa zilizopo katika Muungano.
Sehemu ya wanafunzi kutoka Vyuo vya Elimu ya Juu vilivyopo mkoani Dodoma wakifuatilia hotuba ya ufunguzi kutoka kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba. Kongamano hilo limefanyika katika Chuo cha Mipango Dodoma na kuhudhuriwa na wanafunzi kutoka Vyuo vya Hombolo, Chuo cha Elimu ya Biashara, St. John, Chuo cha Mipango, Chuo cha Madini na Chuo Kikuu cha Dodoma.
Waratibu wa kongamano hilo, kutoka kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Muungano Bi. Lupy Mwaikambo, Bw. Sifuni Msangi Kaimu Mkurugenzi Idara ya Muungano na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhandisi Joseph Malongo wakifuatilia hotuba ya ufunguzi kutoka kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...